RAIS DKT. MWINYI AMEKABIDHIWA TUZO NA RAIS WA UFARANSA

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ametunukiwa Tuzo ya Juu ya Heshima inayofahamika kama “Legion d’ Honner” na Rais wa Jamhuri ya Ufaransa Emmanuel Macron kutokana na mchango wake mkubwa wakati akiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa la Tanzania. Rais Dk. Mwinyi alitunukiwa Tuzo hiyo leo